Tanzania Safari Channel


1.1 by Tanzania Broadcasting Corporation
Oct 24, 2020

About Tanzania Safari Channel

The official Tanzania Safari Channel Mobile application.

Chaneli ya Utalii (Tanzania Safari Channel) ilizinduliwa rasmi na Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 15/12/2018.

Lengo la kuanzisha Chaneli hii ni kukuza utalii wa ndani na nje na halikadhalika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa uhifadhi.

Maudhui ya Chaneli hii yanalenga kuangazia maeneo ya uhifadhi kama vile: Wanyama wa porini, Viumbe wa Baharini, Misitu, Fukwe, Miamba na Majabari, Utamaduni, Malikale, Michezo, Kumbi za Mikutano na mengineyo.

Madhumuni ya Chaneli hii ni pamoja na:

i. Kuwawezesha Watanzania kuona na kubaini vivutio mbalimbali vilivyoko katika maeneo yote nchini;

ii. Kuwahamasisha wananchi wajenge utamaduni wa kutembelea maeneo yenye vivutio nchini;

iii. Kutangaza duniani vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii kutoka nje ya Nchi;

iv. Kuieleza na kuikumbusha Dunia kwamba Mlima Kilimanjaro, Hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro na hata Zanzibar vipo Tanzania;

v. Kuhamasisha wananchi kutunza, kuenzi na kudumisha tamaduni za asili;

vi. Kuangazia na kuibua fursa mbalimbali zilizopo kwenye mnyororo wa biashara katika Sekta ya Utalii; na vii. Kuyaenzi maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere, aliyoyatoa mwaka 1961, kwamba “sisi sote tuna jukumu kubwa la kulinda na kuhifadhi vivutio vya utalii kwa manufaa ya vizazi vilivyopo na vijavyo”.

Additional APP Information

Latest Version

1.1

Uploaded by

Jose Napz

Requires Android

Android 4.2+

Show More

Use APKPure App

Get Tanzania Safari Channel old version APK for Android

Download

Use APKPure App

Get Tanzania Safari Channel old version APK for Android

Download

Tanzania Safari Channel Alternative

Get more from Tanzania Broadcasting Corporation

Discover